PIUS B. NGEZE

BIOGRAPHY




No video uploads for Pius B. Ngeze
Siri ya Binaadamu Kuishi Miaka Mingi

Kitabu hiki kimezingatia mapinduzi ya Sayansi na Teknolojia, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Matibabu na uelewa uliopo duniani kuhusu elimu mpya ya kumwezesha binadamu kuishi miaka mingi. Ni kitabu cha aina yake ambacho kila mwanadamu anayependa kuishi miaka mingi anapaswa kukimiliki, kukisoma na kukirejea mara kwa mara.


  • Published : January 18, 2021

Jifunze Kustawisha Mboga

Kitabu hiki kimeandikwa ili kiwasaidie Wakulima, Maofisa Ugani, Wanafunzi na Wanavyuo kuanzisha aina mpya ya kilimo, yaani, Ustawishaji wa Mbogamboga. Kutokana na wingiwa aina za mbogamboga zilizopo, kitabu kimeandikwa kwamuhtasari.


  • Published : January 18, 2021

Jifunze Kustawisha Uyoga

Uyoga ni zao la viumbe hai viitwavyo kuvu. Kwa watu wengi hapa nchini Uyoga unaofahamika ni ule unaookotwa au unaoonekana ukiota porini au kwenye vichuguu wakati wa msimu wa mvua. Ukiwaeleza kuwa uyoga hustawishwa kama ilivyo kwa mazao mengine, hawakuelewi!


  • Published : January 18, 2021

Kanuni za Ukulima wa Kisasa

Kanuni za Ukulima wa Kisasa ni kitabu kinachoeleza Kanuni Ishirini na Tano (25) za Ukulima wa Kisasa. Kanuni hizo ni zile ambazo wakulima wanapaswa kuzisoma na kuzielewa kwa lengo la kuendesha kilimo cha kisasa cha mazao mbalimbali ya kilimo. Kanuni hizo zimeelezwa kwa kikamilifu kitabuni.


  • Published : January 18, 2021

Kilimo Bora cha Maharage

Kilimo Bora cha Maharage ni kitabu kinachoeleza asili, historia, umuhimu wake, sehemu kuu za mmea, aina na jinsi ya kulistawisha kisasa ili kuongeza mavuno kutoka magunia mawili kwa hekta hadi zaidi ya magunia kumi na moja kwa hekta.


  • Published : January 18, 2021

Kilimo Bora cha Mahindi

Kilimo Bora cha Mahindi ni kitabu kinachoeleza mambo mbalimbali yanayohusu mahindi: asili yake, ustawishaji, ulinzi, uvunaji na hifadhi yake. Mahindi ni nafaka muhimu nchini. Hutumiwa na wananchi wengi kwa chakula, kuuza na kutengenezea pombe. Watu wengi hupenda kula ugali wa mahindi. Ni mtamu na huleta afya. Lakini, watu wachache wanaojua jinsi ya kustawisha vizuri zao hili. Kitabu hiki kitakuwa cha msaada kwa wakulima, maofisa ugani, wanafunzi na wanavyuo.


  • Published : January 18, 2021

Kilimo Bora cha Muhogo

Kilimo Bora cha Muhogo ni kitabu ambacho kinaeleza asili, aina, historia ustawishaji Muhogo.


  • Published : January 18, 2021

Kutengeneza na Kutumia Mboji Katika Kilimo

Kitabu hiki kinahusu Mbolea za Asili. Mbolea za asili hutokana na viumbe hai, yaani, wanyama na mimea. Virutubisho vilivyo katika mbolea hizi vilitumika kwanza katika kustawisha mimea hiyo au katika kulisha wanyama hao


  • Published : January 18, 2021

Migomba Uanzishaji na Utunzaji wa Shamba

Migomba: Uanzishaji na Utunzaji wa Shamba ni kitabu kinachofundisha mkulima mpya, na hata mwenye uzoefu, namna ya kuanzisha shamba jipya la migomba na kulitunza vizuri. Kitabu kinaeleza pia asili na historia ya zao hili, botania ya mmea, uvunaji na uuzaji wa ndizi. Kitabu hiki kimegawanyika katika sura kumi zifuatazo:


  • Published : January 18, 2021

Misingi ya Kilimo Bora

Ili tuweze kuleta Mapinduzi ya Kijani nchini, lazima kilimo chetu kihame kutoka Kilimo cha Mazoea ambacho kimetumika tangu mababu na mababu, karne na karne na kuwa Kilimobiashara.


  • Published : January 18, 2021

FREE BOOK
Mwongozo wa Kilimo Bora cha Alizeti

Alizeti ni moja ya mazao makuu ya biashara yanayostawishwa hapa nchini. Mbegu zake hutoa mafuta asilimia 35-45 na mashudu yake hutumika kulisha mifugo. Mafuta daraja la kwanza hutumika kupikia chakula cha binadamu na ya daraja la pili hutumika viwandani kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile sabuni, rangi, vipodozi mbalimbali n.k.


  • Published : January 18, 2021

Utengenezaji na Matumizi ya Mboleavunde Katika Kilimo

Mboleavunde ni mbolea inayotengenezwa na wakulima kutokana na masalia ya mimea na wanyama ambayo yameozeshwa na vidubini vilivyo katika rundo. Rundo hilo ni mchanganyiko wa masalia mengi ya mimea na wanyama na katika mahali padogo ambapo vitu hivyo huoza kwa muda mfupi


  • Published : January 18, 2021

FREE BOOK
Jifunze Kustawisha Viazi Mviringo

Katika kundi la mazao ya mizizi, Viazi Mviringo ni maarufu na vina umuhimu wa pekee.Ni zao la chakula na biashara katika nchi nyingi zilizoendelea na zinazoendelea. Zao hili nimoja ya mazao manne yachakula yanayozalishwa kwawingi na kutumiwa na watu wengi duniani.


  • Published : January 18, 2021

Visumbufu Vya Mazao Shambani

Visumbufu vya Mazao Shambani ni kitabu kinachoeleza visumbufu vinavyoshambulia mimea ya mazao ikiwa shambani. Visumbufu hivyo ni vingi, lakini, vinavyozungumzwa kitabuni ni vile muhimu zaidi. Kitabu kimegawanyika katika Sura sita zifuatazo:


  • Published : January 18, 2021

Uboreshaji wa Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji

Uboreshaji wa Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji ni kazi inayohitaji Maarifa na Juhudi ili kupata mazao mengi na yaliyo bora. Wanunuzi hupenda kuku bora, mayai bora na nyama bora ambayo hupatikana kutokana na juhudi ya mfugaji kuweza kuwatunza kuku wake ipasavyo. Ufugaji bora wa kuku humhitaji mfugaji kuelewa na kuzingatia kanuni za ufugaji bora kuku. Ni lazima mfugaji wa kuku wa kienyeji awe na elimu hii ili aweze kuendesha shughuli zake kwa usahihi na kwa manufaa ya wateja.


  • Published : January 18, 2021

Ufugaji Bora wa Kuku

Ufugaji bora wa Kuku ni kitabu kizuri ambacho kimetayarishwa kwa makini kwa ajiliya watu ambao tayari wanafuga kuku wa kienyeji na wakigeni (kuku chotara) na wale ambao wangependa kuanza ufugaji wa kisasa wa kuku


  • Published : January 18, 2021

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa Nyuki

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa Nyuki ni kitabu kinachotoa maelezo kuhusu jamii ya nyuki, namna ya kuwafuga, kurina asali, utunzaji na uuzaji wa asali na nta.


  • Published : January 18, 2021

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa Samaki

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa Samaki ni kitabu kinachoeleza namna ya kufugasamaki nchi kavu kwa kutumia mabwawa. Ufugaji wa samaki huweza kumletea mkulima fedha nyingi kuliko watu wanavyofikiri.


  • Published : January 18, 2021

Jifunze Ufugaji Bora wa Nguruwe

Jifunze Ufugaji Bora wa Nguruwe ni kitabu kinachowalenga wafugaji wa nguruwe wa aina kuu tatu zifuatazo:Wafugaji wenye uzoefu mdogo.Wafugaji wa ngazi ya kati wanaoinukia katika ufugaji wa kisasa na wa kibiashara na Wafugaji wakubwa wanaofuga nguruwe kisasa kwa ajili ya kupata faida kubwa. Wafugaji wadogo wanaoanza au waliokwishaanwenza mtaji mdogo au hawana mtaji kabisa na wanaweza kufuga nguruwe na watangundua kuwa ufugaji huu una faida kubwa. Kinunue kitabu hiki ili uelekee kwenye ufugaji wa kisasa na wa kibiashara.


  • Published : January 18, 2021

FREE BOOK
Magonjwa ya Mifugo

Magonjwa ndicho chanzo kikuu cha vifo vya mifugo na umaskini wa wafugaji. Maelfu ya mifugo hufa kila mwaka kutokana na magonjwa. Bila kuugua, mifugo haiwezi kufa .Dhibiti magonjwa ya mifugo ili kuongeza uzalishaji wa maziwa, nyama, mayai, ngozi n.k. na kuondoa umaskini wa wafugaji. Moja ya Kanuni za Ufugaji Bora inawataka wafugaji wadhibiti magonjwa ya mifugo. Lakini, magonjwa yana visababishi au wakala. Tukijua visababishi hivyo na namna ya kuvidhibiti au kuvipunguza, magonjwa yatapungua . Magonjwa yanazuilika. Magonjwa yanatibika. Tufanye, basi, kazi hizo mbili ili kuboresha ufugaji. Lengo kuu la kitabu hiki ni kuwasaidia wafugaji wafanye hivyo.


  • Published : January 18, 2021

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa Mbuzi

Mwongozo wa Ufugaji Bora wa mbuzi ni kitabu ambacho kinaeleza namna ya kisasa ya kufuga mbuzi na kupata faida kubwa kutokana na ufugaji huo


  • Published : January 18, 2021

Silaha Mia Moja za Kiongozi

Kiongozi ni mtu yeyote, mwanamke au mwanaume, mwenye madaraka au mamlaka juu ya mtu mmoja au watu wengi. Maana nyingine ya Kiongozi ni mtu aliyepewa jukumu la kuongoza mtu mmoja au watu wengi. Mtu mmoja huyo anaweza akawa mwanandoa mwenzie au mtu mmoja mwingine ambaye ana ushirika naye.


  • Published : January 18, 2021

The One Hundred Weapons for a Leader

A leader is any person, a man or woman, with power or authority over one or more people. Another meaning of a leader is a person who was given an authority to lead a single person or many people. That single person may be a fellow matrimonial partner or a fellow person whom you co-operate with. “Many people” may start from his/her family members up to the whole nation.


  • Published : January 18, 2021


No award found

Ask Pius B. Ngeze anything

Contact Form