BOOK OVERVIEW
Ili tuweze kuleta Mapinduzi ya Kijani nchini, lazima kilimo chetu kihame kutoka Kilimo cha Mazoea ambacho kimetumika tangu mababu na mababu, karne na karne na kuwa Kilimobiashara. Hiki ni kilimo kinachotumia sayansi na teknolojia ya kilimo cha kisasa. Hakitumii tena mbegu za asili bali mbegu chotara ambazo huzaa sana. Ni kilimo kinachotumia kwa wingi mbolea za viwandani na mbolea za mboji. Ni kilimo kinachotekeleza kanuni zote za kilimo cha kisasa ikiwa ni pamoja na matumizi makubwa ya maji kwa kutegemea aina ya mimea ya mazao na majira.
Kitabu hiki, Misingi ya Kilimo Bora, kina misingi 20 ambayo ikieleweka na kutekelezwa na wakulima kikamilifu watakuwa wakiendesha kilimobiashara.
Tunashauri Wakulima, Wanafunzi, Wanavyuo, Viongozi, Maofisa Ugani na Maofisa Kilimo wakisome na wakitumie kuleta Mapinduzi ya Kijani nchini kwa kuendesha kilimobiashara.