EMMANUEL MBOGO

BIOGRAPHY




No video uploads for Emmanuel Mbogo
Malkia Bibi Titi Mohammed

Tamthilia hii inamhusu Bibi Titi Mohamed, mwanamke aliyekuwa mstari wa mbele katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Kama mwanachama wa TANU na kiongozi wa Umoja wa Wanawake,


  • Published : December 16, 2017

FREE BOOK
Nyerere na Safari ya Kanaani

Oktoba, 1966 kulizuka mgogoro mkubwa wa kihistoria kati ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Muhimbili.


  • Published : December 16, 2017

Mtumwa Hadi Siti Binti Saad

Historia ya maisha ya Siti Binti Saad kama yalivyosawiriwa na Shaaban Robert na Nasra Mohamed Hilal, na sasa, katika tamthiliya hii ya kihistoria, itamfunulia msomaji wasifu na safari ya maisha ya mwanamama huyu.


  • Published : December 16, 2017

Sadaka ya John Okello na Mapinduzi ya Zanzibar

Sadaka ya John Okello ni tamthilia ya kihistoria kuhusu mapinduzi ya tarehe 12/1/1964 visiwani Zanzibar.


  • Published : December 16, 2017

Wangari Maathai

Mwaka 2004 Profesa Wangari Maathai, kiongozi wa chama cha kuhifadhi mazingira (Green Belt Movement) nchini Kenya, alitunukiwa tuzo ya Amani ya Nobel kutokana na mchango wake mkubwa katika harakati za kupigana amani, demokrasia, utawala bora, matumizi sahihi ya mazingira na rasilimali kwa manufaa ya kizazi hiki na vizazi vijayo kote ulimwenguni.


  • Published : December 16, 2017

Tanzia ya Patrice Lumumba

KONGO [DRC] ilipata uhuru toka kwa Wabelgiji tarehe 30/06/1960 na Patrice Lumumba akawa Waziri Mkuu wa kwanza. Baada ya miezi sita tu, yaani tarehe 17/01/1961, Lumumba akauliwa kikatili na kinyama.


  • Published : September 1, 2020

Fumo Liongo

Fumo Liongo alikuwa shujaa wa mji wa Pate katika Pwani ya Afrika ya Mashariki aliyeishi kati ya karne ya 9 na ya 13.


  • Published : September 25, 2020

Siri za Maisha

Kama wewe ni mwanafunzi, mwalimu, mfanyabiashara, profesa, msanii, mkulima, fundi, mwanariadha au mama wa nyumbani, unao uwezo wa kubadilisha maisha yako katika nyanja yoyote ile kama unataka.


  • Published : November 23, 2020

Watoto wa Maman’tilie

Katika riwaya hii ya Watoto wa Maman’tilie, mwandishi anathibitisha kuwa mama ni mtu wa muhimu sana. Riwaya inasimulia na kushadidia kuwa Maman’tilie ni nguzo na dereva wa familia yake yenye wasafiri watatu:


  • Published : May 22, 2021

FREE BOOK
Nyerere na Vijiji Vya Ujamaa

Msingi na dafina ya tamthilia hii ni historia na lengo kuu la Mwalimu Julius Nyerere na TANU kutaka kujenga uchumi wa Ujamaa na Kujitegemea mintarafu mwongozo wa kitabu cha Azimio la Arusha, 1987.


  • Published : August 5, 2021

Shujaa Mirambo

Tamthilia hii ya kihistoria inamhusu Mirambo, Mnyamwezi na mtemi wa Urambo toka mwaka 1860 hadi 1884. Mirambo alikuwa mwanajeshi na mtawala shupavu aliyetawala himaya kubwa upande wa magharibi ya Tanganyika. Kwa kutumia jeshi lake la vijana hatari waliojulikana kama Lugaluga [Rugaruga],


  • Published : October 4, 2021

Mwinyi na Manyani ya Adili

Tamthilia hii inaangazia hali ya maisha nchini Tanzania kabla na wakati wa utawala wa Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi (Mhe). Tamthilia inaonesha Rais Mwinyi akipokea dola nchi ikiwa inaning’inia katika mtego mkubwa wa kifalsafa, kisiasa na kiuchumi, mtego uliowaweka wananchi katika lindi la taabu na ufukara usiomithilika.


  • Published : June 5, 2022

FREE BOOK
Julius Nyerere Kizimbani

Tamthiliya hii inahusu tukio la kweli la kihistoria lililotokea mwaka 1958. Katika mwaka huo, TANU ikiwa na umri wa miaka minne pekee, serikali ya kikoloni ilidhamiria kuuyumbisha na hatimaye kuusambaratisha kabisa uongozi wa chama.


  • Published : June 5, 2022

Giza Limeingia

No Description


  • Published : January 5, 2023

Morani

Tamthiliya ya Morani inasawiri misukosuko ya kisiasa na kiuchumi nchini Tanzania katika miaka ya 80. Katika kiwango cha uhalisia, tunamwona Dongo muhusika mkuu, akipambana na wahujumu uchumi....


  • Published : January 5, 2023

FREE BOOK
Kumng'Oa Nduli

Tamthiliya hii inaakisi awamu mbili za utawala wa Dikteta Idi Amin nchini Uganda. Awamu ya kwanza ni kuanzia mwaka 1971 alipomng’oa Milton Obote na kujitangaza rais wa maisha wa nchi ya Uganda.


  • Published : January 5, 2023


No award found

Ask Emmanuel Mbogo anything

Contact Form