EUPHRASE KEZILAHABI

BIOGRAPHY




EUPHRASE KEZILAHABI SEHEMU YA KWANZA

Florida Kezilahabi mke wa Euphrase Kezilahabi akitoa historia ya mume wake kabla ya kuwa mtunzi wa vitabu.


  • Views : 268

EUPHRASE KEZILAHABI SEHEMU YA PILI

Florida Kezilahabi mke wa Euphrase Kezilahabi akitoa historia ya mume wake, safari zake pamoja na utunzi wake n.k


  • Views : 10

Gamba la Nyoka

Gamba la Nyoka ni riwaya inayoonyesha jinsi maamuzi ya kisiasa yasiyotafakariwa yanavyoweza kuwa na athari mbaya kwa wanyonge na wakulima.


  • Published : March 22, 2022

Kichwamaji

Riwaya ya Kichwa Maji ni Riwaya iliyoandikwa mwaka 1974 na E. Kezilahabi. Hii ni Riwaya ya Kisaikolojia kwa sababu inadodosa nafsi ya mhusika, fikra, hisia, mawazo, imani, hofu, mashaka, matumaini na matamanio yake binafsi na athari za mambo hayo kwake na kwa jamii yake.


  • Published : March 22, 2022

Kaptula la Marx

Chanzo ni jaribio la wafungwa gerezani kukusanya habari nyingi za "dunia ya nje" iwezekanavyo kwa kuiangalia kupitia shimo dogo ukutani.


  • Published : March 22, 2022

Dunia Uwanja wa Fujo

“Dunia uwanja wa fujo” inaelezea jinsi maisha yaliyopo duniani ni sawa sawa na fujo kwani kila mtu anayekuja duniani huleta fujo zake na baadae kutoweka.


  • Published : March 22, 2022

Nagona

Nagona ni riwaya fupi ya kifalsafa na kibaadausasa inayoibua fikra juu ya falsafa na maana ya uhai, maisha, dhamiri na hata fikra yenyewe. Mhusika kiini wa novela hii anajikuta katika mazingira ya ajabuajabu katika nyakati tofauti tofauti.


  • Published : June 5, 2022

Mzingile

Mzingile ni novela (riwaya fupi) ya kifalsafa na kibaadausasa iliyochapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1991. Riwaya hii ni pacha ya ile ya Nagona (1990). Riwaya hii inasawiri chimbuko, maendeleo, maangamizi na kuzaliwa upya kwa dunia kutokana na fujo za wanadamu.


  • Published : June 5, 2022

Dhifa

Dhifa ni diwani ya mwisho ya Kezilahabi. Diwani hii inakusanya tungo za miaka ya 1990-2008, wakati wa mageuzi ya kiliberali mamboleo yaliyoasisiwa na Rais Ali Hassan Mwinyi na kuendelezwa na warithi wake baada ya Mwalimu J.K. Nyerere kustaafu.


  • Published : June 5, 2022

Karibu Ndani

Karibu ndani ni diwani ya pili ya Kezilahabi. Hii imekusanya mashairi yaliyohusu harakati za Ujamaa nchini Tanzania, hususani “kushindwa” kwa Ujamaa kutokana na unjozi na upofu wa waasisi wake; mgogoro wa ushairi wa miaka ya 1970 kati ya wanajadi na wanamabadiliko, tafakuri kuhusu maisha ya kawaida, na kuhusu falsafa


  • Published : June 5, 2022

Rosa Mistika

Rosa Mistika ni riwaya inayohusu masaibu ya msichana Rosa aliyelelewa katika mazingira ya udhibiti wa kidini na kimila katikati ya lindi la umaskini; na baadaye akakabiliwa na vishawishi pale alipoingia katika shule ya bweni na kisha chuo cha ualimu.


  • Published : June 5, 2022

Kichomi

Kichomi ni diwani inayoakisi mawazo anuwai kutoka kwenye nyanja tofauti za maisha, kama vile uchumi, siasa, utamaduni, ndoa na dini; hususan katika sehemu ya kwanza ya diwani aliyoiita Mashairi ya Mwanzo.


  • Published : March 18, 2024


No award found

Ask Euphrase Kezilahabi anything

Contact Form