Siku Saba za Mwendawazimu
Publisher
Ape Network
Language
Swahili
BOOK OVERVIEW
SIKU SABA ZA MWENDAWAZIMU ni riwaya iliyosheheni visa mbalimbali vinavyoelezea matatizo yanayojitokeza katika jamii. Katika riwaya hii ya kusisimua, mwandishi anawachora Kikopo na Mfuniko kama wahusika wendawazimu lakini katika hali yao ya uendawazimu, wahusika hawa wakuu pamoja na wahusika wengine wanaonesha ni changamoto zipi wananchi, hasa wa kipato cha chini, wanakabiliana nazo. Mwandishi anazungumzia pia suala la thamani ya maadili na umuhimu wa kujitambua, kukubali na kudumisha utamaduni wetu. Hii ni hadithi iliyojaa kejeli na ucheshi ndani yake. Mwandishi anatumia mbinu hii ya kejeli na ucheshi kuwasilisha ujumbe muhimu kwa jamii.