Kichwamaji
Publisher
Ape Network
Language
Swahili

Rent This Book

Expires on August 04, 2025

TSh 4,000/=

Choose Option

BOOK OVERVIEW

Riwaya ya Kichwa Maji ni Riwaya iliyoandikwa mwaka 1974 na E. Kezilahabi. Hii ni Riwaya ya Kisaikolojia kwa sababu inadodosa nafsi ya mhusika, fikra, hisia, mawazo, imani, hofu, mashaka, matumaini na matamanio yake binafsi na athari za mambo hayo kwake na kwa jamii yake. Mwandishi E.Kezilahabi ameeleza mambo mengi yanayohusiana na jina la kitabu chake kwa kubainisha misukosuko na migogoro mbalimbali ambayo imesababisha kupatikana kwa dhamira zinazoendana na Riwaya hii. Riwaya hii yenye vikwazo, ucheshi na kuamsha hisia za wasomaji, imesheheni mbinu lukuki za uandishi ambazo zimependezesha na kuipa Riwaya hii maana kulingana na mazingira au jamii husika. Mwandishi ametanabaisha aina ya Riwaya hii kuwa ni ya Kisaikolojia kwa kutumia wahusika mbalimbali kwenye Riwaya hii. Katika sura ya pili ukurasa wa 30 na 31, ambapo Mzee Kabenga aliiathiri Kisaikolojia familia ya Mzee Mafuru, kwani alifanya matukio ambayo si ya kawaida kwenye jamii kiasi kwamba wanajamii waliathirika kisaikolojia kwa sababu ya mawazo yale.

COMMUNITY REVIEWS

There are no reviews for this book yet

Write a Review