Karibu Ndani
Publisher
Ape Network
Language
Swahili
BOOK OVERVIEW
Karibu ndani ni diwani ya pili ya Kezilahabi. Hii imekusanya mashairi yaliyohusu harakati za Ujamaa nchini Tanzania, hususani “kushindwa” kwa Ujamaa kutokana na unjozi na upofu wa waasisi wake; mgogoro wa ushairi wa miaka ya 1970 kati ya wanajadi na wanamabadiliko, tafakuri kuhusu maisha ya kawaida, na kuhusu falsafa. Falsafa ya Kezilahabi kuhusu maisha na ulimwengu iliyomo katika kazi zilizotangulia bado inajitokeza katika diwani hii.